Tuesday, 8 April 2014

Chama cha msingi cha ushirika Kyerwa chatoa shilingi laki tano kwa ajili ya miti ya kutunza mazingira.

Mwenyekiti wa KDCU, Ndg. Prosper Murungi



Kyerwa - Kagera

Chama cha msingi cha ushirika cha Kamuli wilayani Kyelwa Mkoani kagera kimetenga fedha zaidi ya shilingi laki tano kwa ajili ya kupanda miche ya miti mbalimbali ili  kuboresha mazingira.
Wakati mvua zikiwa zinaendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali wilayani Kyerwa uongozi wa chama cha msingi cha ushirika kamuli kikiongozwa na mwenyekiti wake Prosper Murungi ambaye pia ni mwenyekiti wa chama kikuu cha ushirika cha wilaya za Kyerwa na Karagwe  KDCU LTD, walitenga kiasi cha shilingi laki tano kwa ajili ya kupanda miti ya aina mbali mbali katika ardhi ya chama hicho kwa ajili ya utunzaji wa mazingira.
                         
Murungi amewaelekeza wakulima katika ushirika huo kuwa njia pekee ya kuwa na mafanikio ni kujiunga na ushirika baadae kukopa kwa  malengo  na kurejesha  kwa busara.

Mkutano mkuu katika chama cha msingi cha Kamuli ambao ni kupanga bajeti ya mwaka 2014/2015 uliofanyika hivi karibuni umeridhia mapendekezo  hayo na kufikia sasa mchakato wa upandaji miti unaendelea.


Baadhi ya wanachama walishukuru kuwepo kwa mapendekezo hayo ya kununua miche na kueleza kwamba mazingira yanapopandwa miti huvutia lakini pia miti huvuta mvua katika eneo ambapo inakuwa imepandwa.

Vyama vya msingi vya ushirika wilayani Kyerwa vinajihusisha na ununuzi wa zao la kahawa ambalo ni zao la biashara katika wilaya za Kyerwa na Karagwe.



No comments:

Post a Comment