mpango huo usizae matunda kutokana na changamoto zinazokabili sekta ya elimu wilayani Karagwe mkoani Kagera.
Hayo
yalisemwa na wadau mbali mbali wa elimu wakati walipokuwa katika majadiliano
katika maadhimisho ya wiki ya elimu yaliyofanyika kiwilaya katika kata ya
Kituntu wilayani humo hapo jana ambapo kwa upande wa wilaya ya Karagwe
walipanga kuhitimisha siku hiyo April 08 mwaka huu.
Afisa
elimu shule za msingi wilayani Karagwe Gidioni Mwesiga akiwa katika maadhimisho
hayo alisema kuwa, ili kuhamasisha walimu juu ya mpango wa matokeo makubwa sasa
watazunguka katika shule zote za msingi wilayani humo wakitoa mafunzo juu ya
mpango huo na umuhimu wake.
Akiongea
na gazeti hili Gidion Mwesiga ambaye ni
Afisa elimu shule za msingi wilayani humo alisema, kuna changamoto ya uhaba wa
walimu ambapo halmashauri ya wilaya ya karagwe inahitaji walimu 1929.
Mwesiga
alisema kuwa,wanao upungufu wa walimu 628 uwiano kwa mwalimu mmoja anafundisha wanafunzi
62 na serikali kwa mwaka huu ilituma
walimu 157 wakiripoti watakuwa na upungufu wa walimu 471.
Aliongeza
kuwa changamoto hizo wao kama uongozi watazijadili na walimu, wanafunzi na wazazi
ili ziweze kutatuliwa na hatimaye kuwa na wanafunzi wanaopata elimu bora
wilayani humo na si bora elimu.
Vile
vile alizitaja changamoto mbali mbali zinazokabili elimu katika wilaya yake
kuwa ni pamoja na shule kutokaguliwa kwa wakati kutokana na ofisi ya ukaguzi
kutokuwa na fedha ambapo kushindwa kukaguliwa kwa shule kunasababisha kutokuwa
na kipimo bora juu ya elimu.
Alizitaja
changamoto nyingine kuwa ni kupata fedha kidogo ya ruzuku ya uendeshaji wa
shule
(capitation grant), fedha ambayo haikidhi mahitaji ya shule.
(capitation grant), fedha ambayo haikidhi mahitaji ya shule.
No comments:
Post a Comment